Social Icons

Pages

Friday, September 17, 2010

MAPACHA WANAO FANANA SURA MPAKA TABIA....


Kulwa,Dotto na Tatu...ni mapacha ambao wana fanana saaaaaana kuanzia sura mpaka tabia,ni marafiki wakubwa ambao hawaachani kila wanakokwenda. Wanawachanganya hadi wazazi wao kwa kushindwa kuwatofautisha kuwa nani ni nani kwa jinsi wanavyorandana,kama mmoja akihisi njaa basi wote wanakuwa hivyohivyo,akiumwa mmoja basi wote inakuwa hivyo n.k. Sasa swali ni kwamba, vipi wakifikia umri wa kuolewa itakuwajeeeeeeeee? Maana hawaachani hata kwa sekunde 1.Mmmmh! Mi mgeni jamani lol!

Wanapendana sana kiasi kwamba kila jambo wanalitenda kwa pa1. Mamayao ilimlazimu kuvunja choo na kukitengeneza upya kwa ufinyu ili angalau kuikomesha tabia ya mapacha hawa kuingia chooni pamoja kama mmoja wao akibanwa na haja..mmmh, kaazi kweli kweli.

Mama na Watoto wake..yani safiiiiii mpaka raha.

Hawa watoto bwana! Hahha hahh hha..hata kama nguo ni moja ni lazima waifue wote kwa pamoja..duuuh!!

Hii ndo biashara(Kufuga nguruwe na kuuza) anayo jishughurisha nayo mama watatu ili kuweza kuwasomesha watoto wake na kuhakikisha wanapata mahitahi yote.

Mmmmh! Mwenzngu, hebu nionyeshe Kulwa,Dotto ama Tatu yu wapi hapa? Maana mi wamesha nichanganya hawa warembo lol!..

4 comments:

  1. wanapatikana wapi? they are really cute. it happened to twins girls. when one wanted to marry a guy, the other insisted on the same man. parents had nothing to say or do other than allowing the guy to 'get two for the price of one'

    ReplyDelete
  2. inimewapenda hawa watoto mpaka nashindwa kujizuia kurudi hapa kibarazani kuuliza mwathwali mengine.

    umri, shule wanasoma, marafiki zao, wanapendelea nini, hawapendi nini.

    ila huyo wa katikati mwenye jaketi la kijani anapenda kutabasamu zaidi kuliko kucheka. naanza kuwatofautisha

    ReplyDelete
  3. wangekuwa watoto wa matajiri tayari tungewana kwenye magazeti ya kiu, sani na mengine kama hayo.

    na mimi nimezidi eeh

    ReplyDelete
  4. Walizaliwa Septemba 4, 1997. MANENO YAO NI HAYA KAKA (Tunao marafiki, lakini sisi ndiyo marafiki wakubwa, hatupendi kuachana na tunamuomba Mungu tukihitimu darasa la saba tupangwe shule moja tena ya kulala huko huko,”,WANAISHI NJOMBE,MTAA WA CHAUGINGE) AHSANTE SANA KAKA KWA KUVUTIWA NAO NA PIA WANAHITAJI MSAADA SO KUPITIA BLOG YAKO NAWE WAWEZA WASAIDIA PIA....AHSANTE

    ReplyDelete

 

Sample text

Sample Text