Mtu na chama chake bana, bendera ya chama chako unaiweka popote unapo jisikia ili mradi pawe panapo kuhusu. Hapa ni Migoli Mtera kulikuwa na mkutano ulioendeshwa na wana chama wa CHADEMA wakishirikiana na wananchi wa Migoli kujadili kuhusu Katiba mpya.
Hii picha niliipiga kwa mbaliii na kilichonivutia ni huyo dada upande wa kushoto alivyo chomeka chanuo kunako nywele, ni style ya zamani lakini vijijini bado wanaiendeleza sijajua kama alikuwa anataka akasuke ama ndo aliamua kuwa hivyo kwa siku hiyo. Pole mpendwa wangu picha haionekani vizuri.
Watoto bwana, ukikaa na kuwafuatilia kuanzia asubuhi mpaka jioni unaweza usiwaelewe lakini wenyewe waelewana kwa kila kitu wanachokifanya ama kuongea, mi huwa nafurahi tu na sifa na utukufu kumrudishia muumba, maana huu ni uweza wake.
No comments:
Post a Comment