Monday, May 21, 2012
NIMEJIKUTA NIPO SALE NA MKWE LEO... HAH HAHH
KUTOKA MIGOLI MTERA, ZILINIVUTIA TU...
Friday, May 18, 2012
KILA MTU ANA MBINU ZAKE ZA USAKAJI MAHELA
Kila mtu analiwazo lake bana haswa pale anapokuwa na msongo wa mawazo, baba huyu anaekaa maeneo ya kitanzini Iringa Mjini ye liwazo lake ni hili gitaa lake, akishamaliza mishe zake za usakaji mshiko akili inakuwa imechoka kifaa pekee kinachoweza kufanya akawa sawa ni hili gitaa na analikung'uta haswaa, wanaoguswa na nikuno yake basi kumtunza hailipiwi... Mi pia ni mmoja wawalio pagawishwa nauchanaji nyuzi wake... Chukua hiyooo!!!

Wakati mzuka wa gitaa umepanda akaja mama muuza vibatari, baba huyu akamwuliza bei yake mama akasema 800, dingi huyu akasema ye anaweza kumuungisha kwa mia7, mama akasema hailipi, baba akasema ye hapo ndo anaposimamia. Kijana hapo pembeni ye alienda hapo kusikiliza nyuzi zinavyochanwa na mdingi huyu...
Thursday, May 17, 2012
FURAHI NA WADAU WENZIO
JAMANI HODIIIII!!
Kitambo sana wapendwa wangu niliwasusa, halikuwa kusudio langu ni wingi wa mambo ndo ulinifa ufinyu wa kuwatupia tupia chochote kunako KIDUCHU... Sasa walau mambo yako sawa na nafasi inapatikana si mbaya kama mkaendelea kupata mambo kwa uduchu kupitia hiki kibaraza chetu chakupeana viduchuuuuz, tuliobahatika kuuona mwaka 2012 yatupasa kumshukuru mwenyezi mungu maana ni kwa mapenzi yake mpaka leo hii sisi kuendelea kuvuta pumzi yake pasi na malipo na si kwamba tu wema saaana la hasha, na kwa wenzetu walio tangulia mbele ya haki tuzidi kuziombea roho zao zilazwe palipo pema peponi Aamina, na wagonjwa wote mungu awape uponyaji ili tujumuike kwa pamoja katika kuendeleza ujenzi wa taifa letu. Baada ya kusema hayo yote nawakaribisha tena.


